Psalms 18:20-24


20 a Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu;
sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.

21 bKwa maana nimezishika njia za Bwana;
sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

22 cSheria zake zote zi mbele yangu,
wala sijayaacha maagizo yake.

23 dNimekuwa sina hatia mbele zake,
nami nimejilinda nisitende dhambi.

24 e Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu;
sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.

Copyright information for SwhKC